🏟️ AL AHLY 2️⃣-2️⃣ MAMELODI
Hapa Limepigwa Pira Dunia yaani mwendo mwanzo mwisho .
Ila Wachezaji wa Mamelodi Sundowns mguuni wana Sumaku wale Viungo washambuliaji wa moto sana .
Cassius Mailula anasababisha mabao mawili Assist na bao la pili shuti lake liligonga mwamba Morena akatikisa nyavu .
Makoena huyu ni kocha wa Bol haswaa Mamelodi wananikumbusha migusu ya Barcelona Al Ahly wamelala na Viatu mana siyo Kwa pasi Zile .
Yule Allende,Maema na Mailula ufundi mguuni wamebarikiwa wanaufanya Mpira watakavyo .
Aliou Dieng bonge la Kiungo huyu walikuwa na vita nzito na kijana wa Sundowns Makoena pale kati .
Mo Hany anakosa penalty Ronwen Williams anafuta na kuibeba Sundowns huyu ni Moja ya Makipa Bora Africa Kwa sasa
Kwa huu Mpira 😁harafu Kuna timu zipo Bongo zinawaza kubeba Ubingwa huu itakuwa miujiza Kwa sasa .
😁Kwa huu Mpira ndugu zangu na mbio hizi wale wazeee hapa wangetapika ni Bora waliingia mitini walichungulia mbele 😁🏃
Abdelmonem ⚽ (5) Shalulile ⚽ (34)
El Shehat ⚽ (74) Morena ⚽ (80)
No comments:
Post a Comment